Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 44 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 370 2021-06-04

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA K.n.y. MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawasaidia wananchi wa Kigoma ambao wamekuwa wakikamatwa mara kwa mara kwa kuitwa wakimbizi nchini mwao?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Assa Nelson Makanika, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupita Idara ya Uhamiaji imepewa jukumu la kudhibiti, kusimamia na kufuatilia uingiaji, ukaaji na utokaji wa wageni hapa nchini kama ilivyoainishwa katika kifungu cha 12 (1) cha Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54 rejeo la mwaka 2016.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutimiza jukumu hilo, Idara ya Uhamiaji imekuwa ikifanya operesheni, doria na misako mbalimbali kwa lengo la kuwabaini wageni wanaoingia na kuishi nchini kinyume cha sheria na taratibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa ikifanya mahojiano na uchunguzi wa kina ili kujiridhisha juu ya uraia wa watuhumiwa wanaokamatwa wakati wa operesheni husika na kwamba Idara ya Uhamiaji katika kushughulikia masuala ya uraia huzingatia matakwa ya Sheria ya Uraia Sura ya 357 rejeo la mwaka 2002. Operesheni, doria na misako hufanyika kwa mikoa yote na siyo Mkoa wa Kigoma pekee. Nakushukuru.