Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 43 Energy and Minerals Wizara ya Madini 366 2021-06-03

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza:-

Je, nini mpango wa Serikali baada ya kukamilika kwa Mradi wa Utafiti wa Madini ya Graphite Kata ya Chiwata?

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Ndanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilika kwa shughuli za utafiti wa madini ya kinywe katika Kata ya Chiwata ambayo ipo Jimbo la Ndanda, Wilayani Masasi, mpango wa Serikali ni kutoa leseni ambapo hadi sasa leseni mbili za uchimbaji wa kati zimekwishatolewa kwa Kampuni ya Volt Graphite Tanzania Limited.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya kupewa leseni, ni wajibu wa kampuni iliyopewa leseni sasa kuendeleza mradi huo kwa kuanza uchimbaji.