Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 43 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 362 2021-06-03

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Kilosa hadi Mikumi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine G. Ishengoma, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kilosa – Mikumi ni sehemu ya barabara ya Dumila – Rudewa – Kilosa – Mikumi yenye urefu wa kilometa 142.3 ambayo ni ya Mkoa inayosimamiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini TANROADS.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa awamu kama ifuatavyo:-

(i) Ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya barabara kutoka Dumila hadi Rudewa yenye urefu wa kilometa 45 ulishakamilika na barabara inatumika.

(ii) Ujenzi wa kiwango cha lami wa sehemu ya barabara kutoka Rudewa hadi Kilosa yenye urefu wa kilometa 24 ulianza Februari, 2019 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2021.

Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa sehemu ya barabara iliyosalia kutoka Kilosa hadi Mikumi yenye urefu wa kilometa 73.3 kwa lengo la kuijenga kwa kiwango cha lami imeshakamilika. Serikali inaendelea na utafutaji wa fedha za ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu hiyo ya barabara. Ahsante.