Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Water and Irrigation Wizara ya Maji 359 2021-06-02

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itavipatia huduma ya maji safi na salama Vijiji vya Kinyamwenda, Igauri, Matumbo, Itamka na Msimihi katika Jimbo la Singida Kaskazini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhan, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/21 imekamilisha miradi ya maji katika vijiji 7 ambavyo ni Mughamo, Mgori, Ngimu, Sefunga, Ghalunyangu, Kijota na Malolo hivyo, huduma ya upatikanaji wa maji kufikia asilimia 66.4 katika Wilaya ya Singida Vijijini.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 utafanyika utafiti wa kina kwa ajili ya kuainisha maeneo yenye maji ya kutosha chini ya ardhi. Hivyo vijiji vya Kinyamwenda, Igauri, Itamka na Msimihi vitapata maji baada ya kukamilisha uchimbaji wa visima na ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji.

Aidha, kijiji cha Matumbo kitapata huduma ya maji ya uhakika baada ya ukarabati wa mradi wa maji kukamilika mwezi Julai, 2021.