Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 357 2021-06-02

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti mfumuko mkubwa wa bei za bidhaa ulioanza tangu Desemba, 2020 ambao umefanya gharama za maisha kupanda?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mfumuko wa bei ulipanda kutoka asimilia 3.2 mwezi Desemba 2020 hadi asilimia 3.5 mwezi Januari 2021. Hii ilitokana na upungufu wa baadhi ya bidhaa sokoni ambao hutokea mara kadhaa katika vipindi vya mwanzo wa mwaka kama hivyo.

Aidha, mfumuko wa bei ulishuka na kufikia asilimia 3.3 mwezi Februari 2021 ikiashiria kuwa bidhaa na huduma zilianza kupatikana kwa bei nafuu kulinganisha na mwezi Januari mwaka uliopita.

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa mfumuko wa bei unaendelea kubaki ndani ya wigo wa tarakimu moja kati ya asilimia 3.0 hadi 5.0. Lengo hili linaweza kufikiwa kutokana na mikakati mbalimbali ya Serikali ikiwa ni pamoja na kuimarisha usambazaji wa chakula kutoka maeneo ya uzalishaji hadi katika maeneo ya walaji, kuimarisha usimamizi wa Sera ya Fedha na bajeti na kuboresha miundombinu ya barabara za vijijini ili kurahisisha usafirishaji wa mazao kutoka mashambani hadi katika masoko.