Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 354 2021-06-02

Name

Jacquline Andrew Kainja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza:-

(a) Je, Serikali ina mpango wa kuwajengea miundombinu ya kisasa akina mama wa Tabora itakayoweza kukausha mboga kama uyoga, mchicha na majani ya maboga kwa njia ya kisasa zaidi ili kuongeza kipato?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha masoko ya ndani na nje ya nchi ilia kina mama wa Tabora wanaokausha mboga waweze kuuza mboga hizo kwa faida?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Kainja Andrew Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Tabora kama ifuatavyo kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau wa kilimo wakiwemo USAID-kupitia mradi wa Lishe, Shirika la Mpango wa Chakula Dunia (WFP) na JICA kupitia mradi wa TANSHEP imekuwa ikijenga uwezo wa wadau kuhusu matumizi ya teknolojia mbalimbali ikiwemo usindikaji wa mazao ya bustani. Serikali pia inahamasisha matumizi ya teknolojia ya ukaushaji wa mboga kwa kutumia nishati ya jua kwa kuwa teknolojia hiyo ni nafuu na rahisi kutumika ikilinganishwa na teknolojia nyingine.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na FAO inatarajia kutekeleza Mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 7.3 utakaofadhiliwa na Mfuko wa Mazingira wa Dunia ili kuwasaidia kina mama wa Mkoani Tabora na Katavi kuimarisha masoko na kusaidia katika teknolojia ya uhifadhi mazao.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na SIDO na miradi na TANSHEP katika sekta horticulture kuunganisha wakulima na masoko ili kuboresha masoko ya ndani na nje ya nchi. Serikali kwa kupitia SIDO imekuwa ikiwapatia akinamama mafunzo ya ukaushaji wa mazao ili yawe na ubora unaotakiwa. Mafunzo yanalenga kufikia viwango vya bidhaa vinavyotambuliwa katika viwango vya TBS. Aidha, wasindikaji hao watakuwa wakipelekwa kwenye maonesho ya aina mbalimbali kama vilevile nanenane ili kutangaza bidhaa zao. Serikali pamoja na Wizara ya Viwanda kupitia SIDO, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na Umoja wa Wajasiriamali Mkoa wa Tabora wanaendelea kuwatafutia majengo wakinamama ambayo yatatumika katika kusindika na kama display centres. Aidha, SIDO imeandaa mkakati wa kuwaingiza wasindikaji watakaokidhi vigezo katika portal ya SIDO.