Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 42 Policy, Coordination and Parliamentary Affairs Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu 351 2021-06-02

Name

Mohamed Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza:-

(a) Je, ni hatua gani zilizofikiwa kwenye mapambano dhidi ya madawa ya kulevya nchini?

(b) Je, ni watu wangapi wamekamatwa kuanzia mwaka 2019 – 2020 na wangapi wamehukumiwa kifungo?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Suleiman Omar, Mbunge wa Malindi lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Spika, Katika kukabiliana na changamoto ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya nchini, hadi sasa Serikali imechukua hatua zifuatazo;

Mheshimiwa Spika, kwanza imetungwa kwa sheria mpya ambayo ilipitishwa na Bunge lako Tukufu, Sheria ya Kudhibiti Dawa za Kulevya Na.5 ya mwaka 2015. Sheria hiyo, ilianzisha Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kama chombo maalum chenye nguvu ya kisheria ya kukamata, kupekua, kuzuia na kupeleleza makosa yote yanayohusiana na dawa za kulevya.

Mheshimiwa Spika, pili; kwa kushirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kama vile Jeshi la Wananchi wa Tanzania kitengo cha Wanamaji na Jeshi la Polisi, Serikali imeimarishaji operesheni za nchi kavu, anga na majini hasa katika viwanja vya ndege, maziwa na Bahari ya Hindi, ikiwa ni mkakati kwa kudhibiti njia na vipenyo vyote. Pamoja na kuendelea kutoa elimu ya athari za matumizi na biashara ya dawa za kulevya.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Serikali kupitia mamlaka imetambua mitandao mikubwa ya wafanyabiashara wa dawa za kulevya nchini na kubaini njia mbalimbali za usafirishaji. Mkakati huo, umechangia kwa kiasi kikubwa kuziba mianya ya uingizaji wa dawa za kulevya na ukamataji wa dawa hizo.

Mheshimiwa Spika, kwa majibu ya swali (b) kutokana na hatua hizi zilizochukuliwa na Serikali, katika kipindi cha mwaka 2019 hadi 2020, jumla ya dawa za viwandani (Cocaine na Heroin) zilizokamatwa ni kilo 426 na gramu 363. Jumla ya dawa za asili bangi na mirungi zilizokamatwa ni tani 28 na kilo 34. Aidha, katika kipindi cha Januari - Desemba 2020, na Januari - Mei 2021, jumla ya watuhumiwa 124 walikamatwa, kati yao 23 wametiwa hatiani na usikilizaji wa mashauri 40 unaohusisha watuhumiwa 83 unaendelea.