Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 40 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 338 2021-05-31

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawafanya Wabunge kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Ardhi kutokana na ukweli kwamba migogoro mingi ya ardhi na mashamba hupelekewa kesi wao?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu namba 27 cha Sheria ya Mahakama za Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi, Sura Namba 216, baadhi ya watu wenye madaraka kama vile Wabunge, Wajumbe wa Halmashauri za Wilaya, Kata na Vijiji hawana sifa ya kuteuliwa kuwa Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya. Lengo la kifungu hiki ni kuwezesha mgawanyo wa madaraka na utendaji kazi katika Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wabunge ni wawakilishi wa wananchi wote katika maeneo yao endapo Mheshimiwa Mbunge atakuwa Mjumbe wa Baraza la Ardhi, wakati wa kutoa maoni ama maamuzi yanayompa ushindi mwananchi wa upande mmoja na kumnyima ushindi mwananchi wa upande wa pili suala hili linaweza kusababisha malalamiko yanayohusu mgongano wa maslahi kutokana na nafasi zao.

Aidha, Wizara yangu inaendelea kutoa elimu kwa Wajumbe wa Mabaraza ya Kata, Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji na Umma kwa ujumla kuhusiana na taratibu za utatuzi wa migogoro ya ardhi zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.