Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 40 Water and Irrigation Wizara ya Maji 337 2021-05-31

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:-

(i) Je, ni lini ujenzi wa mradi wa katika Kata za Izimbya, Kyaitoke, Ruhunga, Mugajwale, Katoro na Kaibanja utaanza na kukamilika?

(ii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Kemondo, Katerero na Bujugo utaanza na kukamilika?

(iii) Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Karabagaine, Maruku na Kanyangereko utaanza na kukamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imepanga kuanza utekelezaji wa miradi ya maji ambayo itahudumia Kata za Izimbya, Kyaitoke, Ruhunga, Mugajwale, Katoro na Kaibanja katika mwaka wa fedha 2021/2022 na muda wa utekelezaji ni miezi 12 na mradi utakamilika mwezi Juni, 2022.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji Kemondo – Maruku umeanza kutekelezwa ambapo kwa sasa upo katika awamu ya kwanza iliyoanza mwezi Januari, 2021. Utekelezaji wa mradi huu utatumia miezi 18 hivyo utakamilika mwezi Julai, 2022. Kupitia mradi wa Maji Kemondo – Maruku; Kata za Kemondo, Katerero, Bujugo, Maruku, Kanyangereko na Karabagaine zitanufaika.