Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 40 Policy, Coordination and Parliamentary Affairs Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 331 2021-05-31

Name

Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuunganisha mifuko ya mikopo iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuwezesha makundi maalum kupatiwa mikopo kwa urahisi zaidi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia maelekezo yako, lakini pia kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Santiel Eric Kirumba, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwishaona umuhimu na kupitia Mheshimiwa Rais iliagiza na kuelekeza mifuko kuweza kuunganishwa na kufuatia maelekezo hayo, Serikali iliunda kamati ya pamoja iliyohusisha Wizara zote zinazosimamia mifuko hiyo, kwa ajili ya kufanya tathmini ya utendaji wa mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi ili kupima utendaji wa mifuko na programu hizo.

Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilika kwa tathmini hiyo, mapendekezo mbalimbali yametolewa kwa ajili ya kuboresha utendaji wa mifuko na programu za uwezeshaji wananchi ikiwa ni pamoja kuunganisha baadhi ya mifuko yenye majukumu na malengo yanayoshabihiana. Taarifa ya tathmini hiyo inaendelea kufanyiwa kazi ndani ya Serikali kwa hatua zaidi ili hatimaye kuiunganisha na kuongeza tija na ufanisi.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Waziri Mkuu imekwishatekeleza agizo hilo kwa kukamilisha tathmini ya mfumo wa kiutendaji wa mifuko hiyo na baada ya kuunganishwa, mtazamo mpya wa muunganiko wa programu na mifuko husika na utekelezaji wake utaanza baada ya mamlaka kuridhia, asante.