Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 41 Water and Irrigation Wizara ya Maji 347 2021-06-01

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:-

(a) Je, ni kwa nini miradi ya maji katika Mji wa Kakonko kwa muda mrefu haijakamilika?

(b) Je, ni lini Mji wa Kakonko na vitongoji vyake vitapata maji safi na salama ya kutosha?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Buyungu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hadi Desemba, 2020 miradi 15 ilikuwa inatekelezwa katika Wilaya ya Kakonko ambapo miradi 14 imekamilika na inatoa huduma ya maji kwa wananchi, mradi mmoja uliobaki ni mradi wa Kakonko ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 65 na unatarajiwa kuhudumia Mji wa Kakonko pamoja na kijiji cha Kasuga.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji wa Kakonko unatekelezwa na RUWASA kwa kutumia Wataalam wake wa ndani kwa ajili ya kuukamilisha. Utekelezaji wa mradi huu unafanyika kwa awamu ambapo awamu ya kwanza ambayo inahusisha ulazaji wa bomba kilometa 35 na ujenzi wa matanki mawili yenye ujazo wa lita 500 kila moja utakamilika mwezi Desemba mwaka 2021 na kunufaisha Mji wa Kakonko pamoja na vijiji jirani vya Kasuga, Mbizi, Kanyonza pamoja na Kata ya Kiziguzigu yenye Vijiji vya Kiziguzigu, Kibingo, Kiyobera na Ruyenzi.

Mheshimiwa Spika, awamu ya pili itahusu kufanya upanuzi kwa kulaza mabomba urefu wa kilometa 78 kuelekea vijiji vya Njoomlole, Muganza, Kihomoka na Nyakayenzi ambapo itakamilika mwezi Juni, mwaka 2022.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali pia imepanga kujenga miradi mipya katika Vijiji vya Chilambo na Kinonko, ukarabati na utanuzi wa mradi wa Muhange kwenda Muhange Juu na Shule ya Sekondari Ndalichako pamoja na kuchimba visima virefu viwili katika Vijiji vya Chilambo na Nyakiyobe.