Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 36 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 297 2021-05-25

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. LAZARO J. NYAMOGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Makao Makuu ya Polisi ya Wilaya ya Kilolo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lazaro Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua hitaji la ofisi ya Makao Makuu ya Polisi Wilaya ya Kilolo na eneo linalohitajika kujengwa ofisi limeshapatikana na ni eneo la Luganga na lina ukubwa wa hekari 16. Zoezi la kufanya tathmini ili kulipa fidia wananchi limeshafanyika tangu mwezi Julai 2020 kupitia wataalam toka Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo na kupata makadirio ya shilingi 110,092,554.00 zinazohitajika kulipa fidia wananchi hao.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inatafuta fedha kwa ajili ya kulipa fidia wananchi na mara baada ya kuwalipa wananchi fidia kwa mujibu wa sheria na taratibu ujenzi utaanza mara moja.