Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 295 2021-05-25

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE K.n.y. MHE. MWANTUM M. ZODO aliuliza:-

Kada ya Elimu inakadiriwa kuwa na upungufu wa walimu takribani 60,000.

Je, Serikali ina mpango gani wa haraka kukabiliana na changamoto hiyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA - (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Mzamili Zodo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mpango wa Serikali ni kuendelea kuajiri na kujaza nafasi zilizoachwa wazi kwa walimu waliokoma utumishi wao kwa sababu mbalimbali kama vile kufariki, kustaafu na walioachishwa kazi kwa mashauri mbalimbali ya kinidhamu. Aidha, Mwezi Mei 2021 Ofisi ya Rais- TAMISEMI imetangaza ajira 6,949 za walimu wa shule za msingi na sekondari ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa walimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuajiri walimu wa shule za msingi na sekondari nchini kadri ya upatikanaji wa fedha.