Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 50 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 426 2016-06-24

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA A. JUMA aliuliza:-
Kumekuwa na muingiliano wa wananchi kuishi karibu, ndani au pembezoni mwa maeneo ya Kambi za Jeshi kama ilivyo kwenye Kambi ya Chukwani.
(a) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutenganisha maeneo hayo na makazi ya wananchi kwa kuweka mipaka madhubuti?
(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa kushughulikia suala hili mapema ili kuepuka migogoro inayoweza kutokea baina ya Jeshi na wananchi?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (Kn.y WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Jeshi, yale ya makambi, ya mafunzo au vikosi yana mwingiliano mkubwa na wananchi au taasisi zingine. Mwingiliano huu husababishwa na wananchi wenyewe kutoelewa mipaka vizuri, lakini walio wengi huingia kwa kujua na wakati mwingine husaidiwa na wataalam wa Ardhi wa Manispaa na Halmshauri zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili linashughulikiwa kupitia marekebisho ya sheria ili kuimaliza migororo hiyo.
(a) Serikali inaona umuhimu mkubwa kuyatenganisha maeneo hayo yasiwe na mwingiliano na wananchi au taasisi zingiene. Hatua zinazochukuliwa ni kujenga kuta au uzio wa waya kwenye maeneo madogo lakini kuna mpango wa kupanda miti kwenye maeneo makubwa sambamba na kuweka mabango makubwa ya tahadhari.
(b) Serikali kupitia Jeshi, tayari imeanza mikakati ya kupanda miti kwenye maeneo ya kambi. Hivi sasa upo mkakati kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017 wa kuanzisha vitalu vya miti kwenye baadhi ya kambi kwa ajili hiyo.