Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 39 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 323 2021-05-28

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Mtwara Mjini kwenda Msimbati ambako kuna mitambo ya visima vya gesi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mtwara Mjini kuanzia Mangamba – Madimba – Msimbati inayokwenda kwenye visima vya gesi vya Mnazi Bay yenye urefu wa kilometa 35.63 na barabara ya Madimba – Kilambo inayokwenda kwenye Kivuko cha Kilambo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji yenye urefu wa kilometa 16.87 ni barabara za mkoa zinazosimamiwa na Wizara yangu. Barabara hizi zinafanyiwa matengenezo kila mwaka na Wakala wa Barabara nchini Tanzania (TANROADS) na zinapitika wakati wote. Katika mwaka wa fedha ujao wa 2021/2022 zimetengwa jumla ya shilingi milioni 231 kwa ajili ya matengenezo.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hizi pamoja na kuandaa nyaraka za zabuni kwa ajili ya kuzijenga kwa kiwango cha lami. Ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara hizi utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.