Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 37 Water and Irrigation Wizara ya Maji 311 2021-05-26

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:-

Je, ni lini Mradi mkubwa wa Maji wa Kabwe katika Wilaya ya Nkasi utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakangata, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji Kabwe una miundombinu yote kwa ajili ya kutoa huduma ya maji. Miundombinu hiyo ni matanki matatu yenye ujazo wa lita 50,000, lita 10,000 na lita 135,000, vituo vya kuchotea maji 29, nyumba ya pampu ya kusukuma maji na mabomba ya kilometa 10.9. Changamoto iliyojitokeza kwenye mradi huu ni uwezo wa nishati ya umemejua kushindwa kusukuma maji ipasavyo kwenda kwenye matanki hayo, hivyo, kusababisha huduma ya maji kusimama kwa wananchi hususan kipindi cha usiku.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha huduma ya maji kwa wananchi wa Kabwe inapatikana muda wote, Serikali imeamua kubadili mfumo wa umemejua kwa kufunga umeme toka kwenye gridi kupitia REA na kazi hiyo inatarajiwa kukamilika kabla ya mwishoni mwa mwezi Juni, 2021.