Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 50 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 425 2016-06-24

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. JUMAA H. AWESO aliuliza:-
Jimbo la Pangani linakabiliwa na tatizo sugu la maji hususan katika Kata za Mkalamo, Masaika, Mikunguni, Mkaja, Mwera na Bushiri.
Je, ni lini Serikali itatatua tatizo hili ambalo limesababisha kuzorotesha shughuli mbalimbali za kiuchumi kwa wananchi wa kata hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso, Mbunge wa Pangani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo inatekeleza Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji Nchini tangu mwaka 2006/2007. Kwa upande wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani imekamilisha miradi ya ujenzi wa miradi mitano katika vijiji sita vya Madanga, Jaira, Bweni, Kwakibuyu, Mzambarauni na Kigurusimba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2015/2016 kiasi cha fedha shilingi milioni 531.1 zimetengwa kutekeleza miradi ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Pangani ambapo kiasi cha shilingi milioni 55 zimeshapelekwa. Aidha, Serikali ilitekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Mkalamo, Kata ya Mkalamo, Stahabu, Mtango, Mikinguni, Mikocheni na Sange Kata ya Mkwaja, Mwera katika Kata ya Mwera, Kipumbwi Kata ya Kipumbwi na Msaraza Kata ya Bushiri na Masaika Kata ya Masaika kupitia Awamu ya Pili ya
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji inayotarajiwa kuanza Julai 2016. Aidha, fedha zilizotengwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ni shilingi milioni 668.2.