Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 307 2021-05-26

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:-

Je, ni lini Barabara ya Kwamtoro – Sanzawa – Mpendo yenye kilomita 58.2 itajengwa kwa kiwango cha kupitika msimu mzima kwani kwa sasa imekatika kutokana na mvua kubwa na kutojengwa kwa muda mrefu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/ 2021, TARURA Halmashauri ya Wilaya ya Chemba imetenga shilingi milioni 84.04 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara ya Kwamtoro – Sanzawa – Mpendo yenye urefu wa kilomita 23. Ujenzi wa barabara hii unaendelea ambapo matengenezo ya barabara yenye urefu wa kilomita 10, makalvati mawili na drift moja umekamilika. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 42 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara yenye urefu wa kilomita 10 na ujenzi wa makalavati matatu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 pamoja na kazi nyingine Wakala wa barabara za Vijijini na Mijini, umepanga kufanya tathmini ya miundombinu ya barabara zake zote ikiwemo za Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ili kuandaa mpango wa namna bora ya kutoa vipaumbele vya ujenzi na matengenezo ya barabara na madaraja. Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara ikiwemo ya barabara ya Kwamtoro – Sanzawa –Mpendo kwa kadri ya upatikanaji wa fedha ili kuimarisha usafiri na usafirishaji.