Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 35 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 293 2021-05-24

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro kati ya Hifadhi ya Lwafi iliyopo Nkasi Kusini na wananchi wa Vijiji vya Mlambo, King’ombe, Tundu na Kata ya Wampembe?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Pori la Akiba la Lwafi liliwahi kuwa na mgogoro wa Kijiji cha King’ombe ambapo baadhi ya wananchi wake walivamia eneo la hifadhi kwa ajili ya shughuli za kilimo. Hata hivyo, mgogoro huo ulitatuliwa na Serikali baada ya kuchukua hatua mbalimbali zikiwemo wananchi kupewa elimu na kuonyeshwa mipaka halisi.

Mheshimiwa Spika, aidha, mgogoro huo ulikwisha, lakini kuna mgogoro mwingine kwa sasa ambao ni kati ya Msitu wa Hifadhi ya Loasi yaani Loasi River Forest Reserve na Vijiji vya Mlambo, King’ombe na Tundu, ambapo wananchi walivamia msitu huo kwa ajili ya makazi na shughuli za kilimo. Serikali imefanyia kazi mgogoro huo kupitia mapendekezo ya Kamati ya Mawaziri Nane ambapo maamuzi ya mgogoro huo yameshatolewa na utekelezaji wake utafanyika katika bajeti ya mwaka 2021/2022.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa rai kwa Mheshimiwa Mbunge na wananchi wanaozunguka eneo hilo kuendelea kutoa ushirikiano katika kuhimiza, kulinda na kutatua migogoro hiyo inayohatarisha uwepo wa maliasili zinazowazunguka.