Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 284 2021-05-24

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuipunguzia mzigo TARURA kwa kuzihamishia TANROADS barabara za Bulamba – Karukekere – Nakatubai – Igunchi – Mwitende na Busambara - Mugara zilizopo katika Jimbo la Mwibara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mugeta Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mapendekezo ya kupandisha hadhi barabara kutoka barabara za Wilaya na kwenda barabara za Mikoa yanatakiwa kuwasilishwa na kujadiliwa kwenye Vikao vya Bodi ya Barabara ya Mkoa. Endapo Bodi itaridhia mapendekezo hayo, yanatakiwa kuwasilishwa kwa Waziri mwenye Dhamana na barabara ambaye ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi.

Mheshimiwa Spika, hatua inayofuata ni maombi hayo kupitiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi chini ya Kamati ya Kitaifa ya Kupandisha Hadhi Barabara ili kuona kama yanakidhi vigezo na Kamati kuridhia au kukataa kupandishwa hadhi barabara husika. Hivyo, nashauri utaratibu huo ufuatwe katika maombi ya kupandisha hadhi barabara za Bulamba – Karukekere - Nakatubai – Igunchi - Mwitende na Busambara - Mugara zilizo katika Jimbo la Mwibara.