Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 33 Water and Irrigation Wizara ya Maji 282 2021-05-21

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Mradi wa Maji Ruduga – Mawindi ili kuwatua ndoo kichwani akina mama wa Mbarali?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha wananchi wa Wilaya ya Mbarali wanapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza, Serikali ilianza ujenzi wa Mradi wa Maji wa Luduga – Mawindi kwa lengo la kuhudumia vijiji sita vya Kangaga, Mkandami, Itipingi, Manienga na Ipwani kwa gharama ya jumla ya shilingi bilioni. 9.66. Utekelezaji wa mradi huo umepangwa kwa awamu (lots) tano. Kazi zilizopangwa kutekelezwa kwa awamu zote ni ujenzi wa banio la maji, mtandao wa bomba jumla ya kilometa 139, matanki sita yenye ujazo wa lita 150,000 moja, lita 100,000 matatu na lita 75,000 mawili na vituo vya kuchotea maji 119.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa banio la maji, mtandao wa bomba jumla ya kilometa 54 na tanki la kuhifadhia maji la lita 150,000, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji 12. Kwa kazi zilizokamilika wananchi wa Kijiji cha Kangaga wameanza kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 utekelezaji wa mradi utakamilika na huduma ya maji itapatikana katika vijiji vyote na kunufaisha wananchi zaidi ya 26,000. (Makofi)