Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 33 Water and Irrigation Wizara ya Maji 281 2021-05-21

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kusambaza maji kutoka Mradi wa Maji Mhangu – Ilogi katika Kata za Lunguya, Ikinda, Shilela, Sogese na Mega katika Halmashauri ya Msalala?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Msalala, Mheshimiwa Iddi Kassim Iddi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Serikali imeendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Mhangu – Ilogi awamu ya kwanza ambayo ilihusisha ujenzi wa bomba kuu kutoka Mhangu hadi Ilogi umbali wa kilometa 56 kwa gharama ya shilingi bilioni 13.86 na kazi hii inatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi huu kwa awamu ya pili ambayo itahusisha usanifu wa miundombinu ya usambazaji maji na ujenzi wa miundombinu hiyo katika kata zote tano ambapo mradi unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwaka 2022.