Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 49 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 422 2016-06-23

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE (K.n.y. MHE. NEEMA W. MGAYA) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa Malangali ndani ya Wilaya ya Wanging‟ombe na wafanyakazi wa Hifadhi ya Mpanga?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali namba 422, la Mheshimiwa Neema William Mgaya kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Nabu Spika, Hifadhi Mpanga au Kipengere lenye ukubwa wa Kilomita za mraba 1,574 kwa mara ya kwanza ilitangazwa kuwa hifadhi mwaka 2002 kupitia Tangazo la Serikali (GN) Namba 483.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya Oktoba10, 2012 Serikali ilitangaza tena Hifadhi hii kuwa Aifadhi ya Akiba, tangazo ambalo lilioneshwa kuwa kijiji hiki kipo ndani ya hifadhi na hivyo kusababisha mgogoro kati ya wanakijiji, wafanyakazi wa hifadhi pamoja na hifadhi yenyewe kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huu, Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Wanging‟ombe mwezi Februari, 2016, aliunda Tume ya kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huu. Pamoja na timu hiyo, Wizara yangu itakutana na Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii na wadau wote kwa lengo la kufanya mapitio ya matangazo yote mawili ili kupata tafsiri sahihi ya mipaka ya Hifadhi na kijiji kisha kurekebisha kasoro zote zilizojitokeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa jambo hili ni nyeti, naomba kuahidi kulifanyia kazi mapema iwezekanavyo mara baada ya vikao vya Bunge lako Tukufu kumalizika.