Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 30 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 256 2021-05-18

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-

Je, ni lini serikali itakuwa tayari kuanza mradi wa TACTIC ili kufikia Malengo Makuu ya Serikali ya mwaka 2020 – 2025 katika kuboresha miundombinu ya barabara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Uendelezaji Miundombinu katika Miji (TACTIC) unatarajiwa kutekelezwa katika Halmashauri za Miji 45 nchini. Mradi unatarajiwa kutekelezwa na Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa fedha za mkopo wenye masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia. Serikali inaendelea na mazungumzo na Benki ya Dunia kuhusu upatikanaji wa fedha hizo na mradi utaanza kutekelezwa baada ya kukamilika kwa majadiliano na fedha kutolewa.