Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 29 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 249 2021-05-17

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA K.n.y. MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kukabiliana na Waganga wapiga ramli chonganishi na Manabii wa uongo wanaodanganya na kutapeli wananchi kila siku?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khatibu Said Haji Mbunge wa Jimbo le Konde kutoka Mkoa wa Kaskazini Pemba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ina jukumu la kulinda watu na mali zao na kuleta amani na utulivu miongoni mwa jamii ikiwa ni pamoja na kuzuia na kupambana na uhalifu wa aina yoyote ile ili usitokee. Katika kutekeleza majukumu hayo operesheni na misako ya mara kwa mara imekuwa ikifanyika katika kuwakamata waganga wapiga ramli chonganishi na manabii wa uongo wanaodanganya na kuwatapeli wananchi na kuwaletea hasara kubwa na mfarakano katika jamii kwa kuwachukulia hatua mbalimbali kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2020 jumla ya wapiga ramli chonganishi 57 walikamatwa na kufikishwa Mahakamani na kesi zao zipo katika hatua mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, nichukue fursa hii kuwatahadharisha wananchi kujiepusha na waganga wapiga ramli chonganishi na manabii wa uwongo kwani matendo yao husababisha hasara, mfarakano na vifo katika jamii. Pia tuendelee kujitokeza bila uoga kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuhusu vitendo hivyo viovu ili hatua stahiki zichukuliwe kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo.