Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 28 Water and Irrigation Wizara ya Maji 241 2021-05-12

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI atauliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza changamoto ya maji katika Wilaya ya Nkasi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenan, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika; hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Wilaya ya Nkasi ni wastani wa asilimia 48. Katika kutatua changamoto ya huduma ya maji, katika mwaka wa fedha 2020/2021 Wilaya ya Nkasi imeendelea na ujenzi wa jumla ya miradi 12 ambayo ni Kirando, Kabwe, Kisula, Isale, Mpasa, Matala, Kantawa, Sintali, Chonga, Kate, Mtambila na Katongolo ambapo itakamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Juni 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, mradi wa uchimbaji wa visima virefu sita umekamilika katika vijiji vya Ntumbila, Kachehe, Itindi, Lyazumbi, Nkomo II na Milundikwa. Ujenzi wa miundombinu ya usambazaji utafanyika katika mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo utahusisha matanki matatu ya maji yenye ukubwa wa lita 90,000 na lita 45,000 na vituo vya kuchotea maji 23.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Mji wa Namanyere, Serikali inaendelea na uboreshaji wa huduma ya maji kwa kutumia chanzo cha maji cha bwawa la Mfili ambapo kazi mbalimbali zitafanyika ikiwemo ufungaji wa pampu mbili katika bwawa la Mfili, ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 3.9, ulazaji wa mabomba na ujenzi wa tanki la lita 500,000 la kuhifadhi maji. Kazi hizo mradi zinatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai, 2021.