Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 28 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 237 2021-05-12

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri ya Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Bulamba – Bukonyo hadi Masonga yenye urefu wa kilometa 32.23 ni barabara ya mkoa inayounganisha mji wa Nansio na Ziwa Viktoria kupitia vijiji vya Murutunguru - Bukonyo hadi Masonga. Barabara hii inahudumiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS).

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kutambua umuhimu wa barabara hii inaendelea kuiimarisha kwa kuifanyia matengenezo ya aina mbalimbali kila mwaka ili kuhakikisha kuwa inapitika kipindi chote cha mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali ilitenga jumla ya shilingi milioni 757.94 kwa ajili ya kuifanyia matengenezo ya aina mbalimbali barabara hii. Kazi za matengenezo hayo inaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya barabara hii kila mwaka ili kuhakikisha kuwa inaendelea kupitika wakati wote kabla ya kuijenga kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika mwaka ujao wa fedha wa 2021/2022, barabara hii imeombewa shilingi milioni 219.159 kwa ajili ya matengenezo ya vipindi maalum na shilingi milioni 510 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida ya Daraja la Nabili lililopo katika barabara hiyo. Ahsante. (Makofi)