Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 236 2021-05-12

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:-

Je, ni lini barabara za kutoka Rubanga – Isulwabutundwe – Mkoba -Kukuruma – Kamhanga - Kishinda na Mkolani zitatengewa fedha na TARURA kwa ajili ya ujenzi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Musukuma Joseph Kasheku, Mbunge wa Geita Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyotajwa vinaunganishwa na barabara za Mkoba Bridge – Isulwabutundwe – Lubanga yenye urefu wa kilometa 15 na Geita – Isamilo – Mkolani kwa maana ya Busekeseke yenye urefu wa kilometa 18 ni barabara muhimu sana kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2020/2021 barabara hizi zimetengewa jumla ya fedha shilingi milioni 318.83 kwa ajili ya matengenezo ya kilometa 33 na wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa kazi. Kazi zinatarajiwa kukamilishwa mwezi Julai mwaka, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini itaendelea kutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kuzifanyia matengenezo barabara zote zilizopo Wilaya ya Geita Vijijini kwa kulingana na upatikanji wa fedha.