Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 27 Water and Irrigation Wizara ya Maji 227 2021-05-11

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Katerela kwa ajili ya Kata za Kasharunga na Rulanda?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Ahsante. kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jitihada za kuhakikisha wananchi Wilayani Muleba wanapata huduma ya maji, katika mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali imekamilisha miradi ya maji ya Bulembo, Kasharunga, Ruteme, Ilogero na Kyota. Pia, utekelezaji wa miradi ya Nshamba, Kishamba na Kashansha unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Mei, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia RUWASA katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepanga kuanza ujenzi wa mradi wa maji kutoka chanzo cha maji Katerela utakaowanufaisha wakazi wapatao 19,619 katika Kata za Kasharunga na Rulanda. Mradi huu unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi million 700 ambapo utahusisha ujenzi wa chanzo cha maji, ujenzi wa matanki mawili ya maji ukubwa wa lita 200,000 na lita 300,000, ujenzi wa nyumba ya mtambo, vituo vya kuchotea maji 25 na ujenzi wa mtambo wa bomba za maji umbali wa mita 40,130.