Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 27 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 224 2021-05-11

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya Ibungu – Kafwafwa hadi Kyimo itafanyiwa upembuzi yakinifu na kuanza ujenzi kwa kuwa imetajwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Ibungu –Kafwafwa – Kyimo ni barabara ya mkoa yenye urefu wa kilometa 68.2 ambapo kilometa 21.8 zipo Mkoa wa Mbeya na kilometa 46.4 zipo katika Mkoa wa Songwe. Barabara hii ni ya changarawe na udongo na inapita sehemu zenye miinuko mikali hivyo kupitika kwa shida wakati wa mvua kutokana na utelezi. Barabara hii ni muhimu kwa kuwa imekuwa ikitumika katika usafirishaji wa mazao mbalimbali ya chakula na biashara kwa kuwa imepita katika maeneo ya wakulima.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, Ibara ya 55(c)(iv): Chama cha Mapinduzi kiliahidi kuielekeza Serikali kukamilisha/kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara mbalimbali hapa nchini zenye jumla ya urefu wa kilometa 7,542.75 ambapo miongoni mwa hizo ni hiyo Barabara ya Ibungu – Kafwafwa – Kyimo yenye urefu wa kilometa 68.2.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Ibungu – Kafwafwa – Kyimo ili hatimaye iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, kwa kutambua umuhimu wa barabara hiyo Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekuwa ikifanyia matengenezo mbalimbali ili kuhakikisha inapitika majira yote ya mwaka. Ahsante.