Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 25 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 214 2021-05-07

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTA D. NJAU K.n.y. MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:-

Je, nini kimepelekea mkwamo wa mkakati wa ujenzi wa Mji mpya wa Kawe kupitia Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na lini mradi huo utaendelea?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mwezi Agosti, 2013, Baraza la Mawaziri kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa, hususani thamani ile ya ardhi katika eneo la Kawe, ilitoa kibali kwa Shirika la Nyumba la Taifa ili eneo hilo ambalo lilikuwa eneo la Kiwanda cha Tanganyika Packers liendelezwe kuwa mji wa pembezoni (satellite town) na uendelezaji huo ufanyike kwa njia ya ubia kati ya NHC na Kampuni ya Al Ghurair Investments. Kazi zilizoanza kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa miradi miwili ya makazi na biashara yani Golden Premier na Kawe 711 ambayo kwa sasa imesimama ikiwa imefikia asilimia 43 kwa Golden Premier pamoja na asilimia 38 kwa mradi wa Seven Eleven (711).

Mheshimiwa Spika, mkwamo wa utekelezaji wa miradi ya Golden Premier pamoja na Kawe Seven Eleven (711) umesababishwa na uhaba wa fedha uliotokana na Shirika la Nyumba la Taifa kufikia kikomo cha idhini ya kukopa iliyotolewa na Serikali kabla ya mradi wake kukamilika. Hali hii ilitokana na Shirika kuwa na miradi mingi sana kwa wakati mmoja ambayo yote ilitegemea vyanzo vilevile vya mkopo kwa ajili ya utekelezaji wake.

Mheshimiwa Spika, ili kuikwamua miradi hii, Shirika limefanya juhudi mbalimbali ili kupata fedha kupitia vyanzo vingine zaidi ya mikopo. Hata hivyo, Shirika tayari limeanza mpango huu wa kukwamua kwa kumalizia Mradi wa Morocco Square, ambao unakadiriwa kukamilika kufikia mwisho wa mwaka huu 2021. Ukamilishaji wa ujenzi wa mradi wa Golden Premier pamoja na Kawe Seven Eleven (711) unategemea kuanza katika mwaka wa fedha 2021/2022.