Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 25 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 213 2021-05-07

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, ni lini Vijiji na Vitongoji nchini ambavyo havijapatiwa umeme vitapatiwa huduma hiyo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) inaendelea kutekeleza mradi wa kusambaza umeme vijijini Awamu ya III mzunguko wa pili. Mradi huu unatarajiwa kufikisha miundombinu ya umeme katika vijiji vyote 1,974 ambavyo havijapata umeme kati ya vijiji 12,268 vya Tanzania Bara.

Mheshimiwa Spika, mradi huu pia utafikisha umeme katika vitongoji 1,474 ambavyo havijafikiwa na umeme. Mradi ulianza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba, 2022. Gharama ya mradi ni takriban bilioni 1,176.

Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vitongoji ni endelevu. Serikali kupitia REA na TANESCO itaendelea kupeleka umeme katika vitongoji vyote mwaka hadi mwaka kulingana na upatikanaji wa fedha.