Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 25 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 212 2021-05-07

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanya Lugha ya Kiswahili kuwa bidhaa ya kimataifa ili kuendeleza na kukuza utamaduni wetu Duniani?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kumfahamisha Mheshimiwa Mussa Ramadhan Sima Mbunge wa Singida Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuwa, Serikali imeanzisha mipango kadhaa ya kimkakati ya kukifanya Kiswahili kuwa bidhaa ya Kimataifa. Tayari kanzidata ya wataalam wa Kiswahili imeanzishwa na wataalam 1318 wamesajaliwa. Pamoja na hayo, Serikali imenunua vifaa vya kisasa vya mafunzo ya ukalimani kwa vitendo na matumizi ya TEHAMA katika ukuzaji wa Kiswahili ambayo yametumia zaidi ya milioni 181.8.

Mheshimiwa Spika, tayari tunao mpango wa kufundisha Kiswahili kwa wageni kupitia balozi zetu nje ya nchi. Vile vile, Serikali imeboresha na kuimarisha mafunzo ya stadi za kufundisha Kiswahili kwa wageni. Pamoja na kutoa machapisho ya Kiswahili rahisi kwa wataalam wetu, na pia kwa lengo la kusaidia nchi zilizoonesha nia ya kuingiza Kiswahili katika mitaala yao ya Elimu mfano Afrika Kusini, Namibia, Rwanda na Uganda.

Mheshimiwa Spika, afua ya hayo, mwaka 2019; wakati wa Mkutano wa 39 wa Wakuu na Viongozi wa Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika-SADC Serikali ilifanikiwa kukifanya Kiswahili kuwa moja ya Lugha nne rasmi zinazotumiwa wakati wa vikao na mikutano ya nchi hizo. Naombwa kuwasilisha.