Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 25 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 210 2021-05-07

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo Kikuu cha Taifa Kusini mwa Tanzania na Kanda nyingine ambazo hazina Vyuo Vikuu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Thea M. Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, taratibu za uanzishwaji wa Vyuo Vikuu vya Umma hazilengi kuanzisha Vyuo Vikuu vya Kikanda, Kimkoa au Kiwilaya. Vyuo Vikuu vilivyopo nchini, vikiwemo vya Serikali na Binafsi, vinapokea wanafunzi kutoka Kanda zote za Tanzania Bara na Visiwani; na kutoka nje ya nchi. Huu ndio utaratibu wa Vyuo Vikuu Duniani kote. Katika Kanda ya Kusini kuna vituo vitatu vya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) vilivyopo katika Makao Makuu ya Mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma. Aidha, kipo Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Maris STeMMUCO kilichopo Mkoa wa Mtwara na Taasisi ya Uhasibu Tanzania TIA Kampasi ya Mtwara.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa mpango wa Serikali ni kuboresha Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu zilizopo kwa kukarabati na kujenga miundombinu mipya pamoja na kuongeza vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia. Tunafanya hivyo ili kuongeza nafasi za udahili na ubora wa elimu itolewayo na hivyo kukidhi mahitaji ya nchi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.