Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 23 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 197 2021-05-05

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question


MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya kutoka Magu – Bukwimba hadi Ngudu itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili kuu nganisha Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba na Makao Makuu ya Mkoa wa Mwanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Emmanuel Mageni Kasalali, Mbunge wa Sumve ,kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya kutoka Magu – Bukwimba hadi Ngudu ni sehemu ya barabara ya Mkoa yenye urefu wa kilomita 71 inayoanzia Magu – Bukwimba – Ngudu hadi Hungumalwa. Barabara hii nikiunganisha muhimu kati ya Wilaya ya Magu na Kwimba kupitia Isandula (Magu) – Bukwimba – Ngudu – Nyamilama hadi Hungumalwa.

Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha kazi ya Upembuzi yakinifu na Usanifu wa Kina kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Magu – Bukwimba –Ngudu hadi Hungumalwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 71. Kazi hii ilifanywa na Mhandisi Mshauri M/s Advanced Engineering Solution kwa gharama ya shilingi milioni 638.486 na kukamilika mwaka 2019. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha za kugharamia ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati ujenzi kwa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha, Wizara yangu kupitia TANROADS inaendelea kuihudumia barabara hiyo ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/ 2021 jumla ya Shilingi milioni 475.551 zilitengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hii.