Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 196 2021-05-05

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro wa bei ya umeme unaotumika na Watanzania waishio Zanzibar ili kuweka usawa kwa Watanzania wote?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Hassan Omar King, Mbunge wa Jang’ombe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimeendelea kushughulikia suala la bei ya kuuza na kununua umeme baina ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) ili kuupatia ufumbuzi mgogoro huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2020/2021 Timu ya Wataalamu wa Taasisi husika zilikutana katika vikao mbalimbali na kufanya uchambuzi wa kina wa vigezo vilivyohusika katika kupanga bei hiyo ya kuuzia umeme kwa wateja wakubwa wa kununua umeme ikiwemo ZECO. Kutokana na uchambuzi huo, inapendekezwa kuwa vigezo hivyo vipitiwe upya ili kuleta unafuu kwa wateja wa aina hiyo ikiwemo ZECO.

Mheshimiwa Naibu Spika, mapendekezo hayo yaliwasilishwa katika Kamati ya Wizara zinazoshughulikia masuala ya Muungano ili kufanyia kazi mapendekezo hayo na kupata ufumbuzi wa kudumu wa suala hili.