Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 22 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 188 2021-05-04

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza:-

Je ni lini Serikali itajenga barabara inayounganisha Jimbo la Ukonga na Mbagala kwa mkupuo badala ya kujenga kilometa moja kila mwaka ili kuondoa kero ya usafiri kwa wakazi wa Majimbo hayo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kutokana na ufinyu wa bajeti, kuanzia mwaka 2000 Serikali imekuwa ikiijenga barabara hii ya Chanika - Mbande inayounganisha Jimbo la Ukonga na Mbagala kwa kiwango cha lami kwa awamu. Hadi sasa jumla ya kilometa 14.34 kati ya kilometa 19.29 sawa na asilimia 74.5 zimejengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami. Aidha, kilometa 4.95 zilizosalia zitaendelea kujengwa kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.