Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 22 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 187 2021-05-04

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya mpakani kutoka Mtawanya kwenda Nanyumbu kupitia Mpilipili – Mapili –Chikoropola – Lichele – Lupaso hadi Lipumburu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mpilipili – Mapili –Chikoropora – Lichele – Lupaso hadi Lipumburu ni sehemu ya barabara ya ulinzi ya Mtwara – Madimba – Tangazo –Mahurunga – Kitaya – Namikupa hadi Mitemaupinde yenye urefu wa kilometa 365.5. Sehemu ya barabara hii yenye urefu wa kilometa 258.0 imeshafunguliwa na inaendelea kufanyiwa matengenezo ya kila mwaka na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Aidha, Serikali imekuwa ikitenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kuendelea kuifungua barabara hii kwa sehemu iliyobaki yenye urefu wa kilometa 107.3.

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) unaendelea kuiboresha barabara hii kwa kuhakikisha inapitika majira yote ya mwaka ambapo jumla ya kilometa 10.8 zimejengwa kwa kiwango cha lami katika maeneo korofi ya milima ya Mtawanya, Kilimahewa, Mdenganamadi, Mnongodi na Dinyeke. Ahsante.