Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 21 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 174 2021-05-03

Name

Mohamed Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH (K.n.y. MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR) aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuajiri Askari wapya Pamoja na kuleta vitendea kazi vya kutosha kwa Polisi Zanzibar inayokabiliwa na upungufu mkubwa wa Askari kutokana na wengi kufikia umri wa kustaafu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Suleiman Omar, Mbunge wa Malindi kutoka Zanzibar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mgawanyo wa rasilimali watu na vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi pamoja na mambo mengine huzingatia hali ya uhalifu wa eneo husika, jiografia ya eneo, idadi ya watu wanaohudumiwa na Jeshi la Polisi na ikama ya watumishi sambamba na upatikanaji wa vitendea kazi kutoka Serikalini.

Mheshimiwa Spika, uwiano wa askari wa Jeshi la Polisi kwa Raia kimataifa ni askari mmoja kwa raia mia nne hamsini (1:450) hata hivyo kwa upande wa Zanzibar takwimu zinaonesha kuwa uwiano ni askari mmoja kwa raia mia tatu na tisini na mbili (1:392). Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2012 hii inamaanisha kuwa idadi ya Polisi Zanzibar ni wengi ukilinganisha na mahitaji katika kuhudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa vitendea kazi, napenda kukiri kuwa kama ilivyo maeneo mengine ya nchi, kuna uhaba wa vitendea kazi. Serikali itaendelea kuongeza ikama ya watumishi na vitendea kazi kadri nafasi za ajira na fedha zitakavyokuwa zinapatikana. Nakushukuru.