Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 18 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 151 2021-04-28

Name

Jaffar Sanya Jussa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Paje

Primary Question

MHE. JAFAR SANYA JUSSA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itavipatia Vituo vya Polisi vya Paje na Jambiani samani za Ofisi pamoja na magari kwa ajili ya doria?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jaffar Sanya Jussa, Mbunge wa Paje, kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua changamoto ya ukosefu wa samani katika Vituo mbalimbali vya Polisi nchini, ikiwa ni pamoja na Vituo vya Paje na Jambiani kutoka Mkoa wa Kusini Unguja na hii ni kutokana na ufinyu wa bajeti. Aidha, Serikali imekuwa ikishirikiana na wadau werevu wa ulinzi na usalama ili kuhakikisha Vituo vya Polisi vinapata samani za kisasa ili kuongeza ufanisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kituo cha Paje wadau werevu wamechangia meza sita, viti kumi na nne na makabati manne. Pia katika Kituo cha Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja wamechangia meza tatu, viti sita na mabenchi mawili na wameahidi kuchangia ama kuendelea kufanya hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali inatambua pia umuhimu wa vyombo vya usafiri katika kutekeleza majukumu ya Jeshi la Polisi. Jeshi la Polisi linatarajia kupata magari kwa ajili ya kutendea kazi na pindi yatakapofika yatatengwa kwenye maeneo yenye uhitaji wa magari na Vituo vya Paje na Jambiani vitazingatiwa zaidi. Nashukuru.