Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 15 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 125 2021-04-22

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza:-

(a) Je, kwa nini barabara ya Mpanda – Ulyanhulu – Kahama haikujengwa katika kipindi cha 2015 – 2020 kama ilivyoelekezwa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015 - 2025?

(b) Je, ni lini sasa ujenzi wa barabara hiyo utaanza kama ilivyoelekezwa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020 – 2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu swali la Mheshimwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Ulyanhulu, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mpanda – Ugala – Kaliua – Ulyanhulu yenye urefu wa kilometa 457 inayounganisha Mikoa ya Katavi, Tabora na Shinyanga ni moja ya barabara zilizopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020. Barabara hii ipo kwenye kundi la miradi inayotakiwa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Mheshimiwa Spika, mkataba kwa ajili ya Upembuzi yakinifu na usanifu wa awali wa barabara ya Mpanda – Ugala – Kaliua – Ulyankulu – Kahama ulisainiwa tarehe 18 Agosti, 2020 kati ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Kampuni ya Crown Tech Consult Ltd kwa gharama ya shilingi milioni 940.30. Kazi hii itafanyika ndani ya miezi 12 na inatarajiwa kukamilika Septemba, 2021. Mara baada ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa Kina kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiendelea, Wizara yangu kupitia TANROADS, inaendelea kuihudumia barabara hiyo ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Aidha, ninapenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kuwa ili ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ufanyike, hatua mbalimbali hufuatwa ambazo ni pamoja na upembuzi yakinifu, usanifu wa kina, utayarishaji wa nyaraka za zabuni na taratibu za ununuzi wa kumpata mkandarasi wa ujenzi. Hivyo, kuanza kwa hatua tajwa, maana yake ni kuanza kwa mradi husika. Ahsante.