Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 14 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 120 2021-04-21

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. SILLO D. BARAN aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Dareda – Bashnet – Dongobesh kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sillo Daniel Baran, Mbunge wa Babati Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Dareda – Bashnet hadi Dongobesh yenye urefu wa kilometa 54 ni barabara ya Mkoa inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania- TANROADS ambapo kilometa 10 zimejengwa kwa kiwango cha lami na kilometa 44 ni za changarawe. Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Dareda – Bashnet hadi Dongobeshi kwa kiwango cha lami. Kazi hii ilifanywa na Mhandisi Mshauri Luptan Consults Ltd kwa kushirikiana na Mhandisi Consultancy Ltd kwa gharama ya shilingi milioni 398. Kwa sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati ujenzi kwa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha, Wizara yangu kupitia TANROADS inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi milioni 513.594 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hiyo. Ahsante.