Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 115 2021-04-21

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:-

Je, ni lini barabara ya kutoka Kilando – Katete – Kazovu – Korongwe katika Wilaya ya Nkasi itakamilika?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa Rukwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabaraya Kirando – Korongwe ina urefu wa kilomita 35. Matengenezo ya barabara hii yalianza mwaka wa fedha 2017/2018 kwa kuanza na usanifu wa barabara yote ya kilomita 35 na usanifu wa daraja moja la mita 40 la Mto Kavunja; Usanifu wa madaraja mawili yenye urefu wa mita 12.6 kila moja.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2016/2017, TARURA ilifungua Barabara ya Kirando – Kazovu yenye urefu wa kilomita 22 iliyotengenezwa kwa gharama ya shilingi milioni
108.37. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, kiasi cha shilingi milioni 11.4 zitatengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara yenye urefu wa kilomita 11.4.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/ 2019, Serikali ilianza ujenzi wa daraja la Mto Kavunja lenye urefu wa mita 40 kwa gharama ya Shilingi bilioni 1.76 na shilingi milioni 954.70 zimeshapokelewa na ujenzi unaendelea ambapo daraja hili linatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2021. Vilevile, katika mwaka wa fedha 2021/2022, daraja hili litatengewa kiasi cha shilingi milioni 500.

Aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara na madaraja yaliyobaki kwenye Barabara ya Kirando – Korongwe kulingana na upatikanaji wa fedha ili kuondoa changamoto ya usafiri kwa wananchi wa Kazovu, Kitete na Korongwe katika Wilaya ya Nkasi.