Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 113 2021-04-20

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Makamu wa Rais kwa Wananchi wa Mbinga ya kujenga barabara ya Mbinga – Litembo – Kigonsera hadi Matiri kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Liuka Kapinga Beyana, Mbunge wa Mbinga Vijiji kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) tayari imeanza kutekeleza kwa awamu mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara tajwa kwa kuanzia na sehemu ya Mbinga – Mbuji – Litembo yenye urefu wa kilometa 24. Hadi sasa jumla ya kilometa 4.89 zimekwishajengwa kwa kiwango cha lami. Kazi hiyo itaendelea kwa awamu kila mwaka kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, wakati Serikali ikiendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami, barabara hii itaendelea kufanyiwa matengenezo mbalimbali ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi milioni 674.896 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu barabara ya Kigonsera – Matiri hadi Kilindi yenye urefu wa kilometa 35.32, Serikali inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ili iweze kupitika majira yote ya mwaka.