Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 12 Water and Irrigation Wizara ya Maji 103 2021-04-19

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY K.n.y. MHE. ZAKARIA P. ISSAAY aliuliza:-

Je, ni lini Wakala wa Maji Vijijini atachimba visima sita katika Vijiji vya Aicho, Gidamba, 7 Gunyoda, Silaloda, Boboa na Titiwi katika Jimbo la Mbulu Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zakaria Paulo Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kazi ya kuchimba visima kwa ajili ya kutumika kama vyanzo vya maji inafanyika maeneo mengi hapa nchini hivyo ili kuepuka ucheleweshaji inabidi kushirikisha makampuni binafsi kuchimba visima baada ya Wataalam wa Mabonde kufanya utafiti na kuainisha maeneo yenye maji chini ya ardhi. Hivyo, kazi hii zabuni imetangazwa kupitia Bodi ya Zabuni ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira ya Mkoa - Babati (BAWASA) ambapo Visima virefu vitatu katika vijiji vya Aicho, Boboa na Titiwi vitachimbwa kuanzia mwezi Mei, 2021 na kukamilika mwezi Juni, 2021.

Mheshimiwa Spika, visima vilivyobaki katika vijiji vya Gidamba, Silaloda na Gunyoda vitachimbwa katika mwaka wa fedha 2021/22.