Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 95 2021-04-19

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza:-

Je, ni lini warithi wa askari E.152 (Makame Haji Kheir) aliyefariki tangu Mwaka 2003 akiwa mtumishi wa Jeshi la Polisi Kituo cha Madema watapewa mafao yake?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haji Makame Mlenge Lengelenge, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma na Ofisi ya Polisi Kamisheni ya Polisi Zanzibar hazijapata kumbukumbu za maombi ya mafao wala nyaraka za mirathi kumhusu Askari tajwa hapo juu kutoka kwa msimamizi wa mirathi. Aidha, kwa sasa Jeshi la Polisi Kamisheni ya Zanzibar limeshafanya jitihada ya kufanya mawasilinao na msimamizi wa mirathi ndugu Mlenge Haji Kheir ili kupata nyaraka zinazohusiana na maombi ya malipo ya mafao ya mirathi ya askari huyo ili ziweze kushughulikiwa. Ahsante.