Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 91 2021-04-16

Name

Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Primary Question

MHE. AHMED YAHYA ABULWAKIL aliuza:-

Je, ni lini Serikali itawaunga mkono wananchi wa Chukwani waliojitolea kujenga Kituo cha Polisi cha ghorofa moja kwa kumalizia ujenzi wa kituo hicho?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Yahya Abdulwakil Mbunge wa Kwahani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Kituo cha Polisi Chukwani ulianza mwaka 2015 na unatekelezwa kwa mchango wa nguvu za wananchi na wadau werevu wa Ulinzi na Usalama huku Jeshi la Polisi likitoa wataalam wa ushauri na usimamizi kwa mafundi wake. Gharama ya ujenzi inatarajia kufikia kiasi cha shilingi 98,000,000/= hadi kukamilika kwake. Kwa sasa ujenzi umefikia hatua ya kumalizia (finishing) na gharama za kumalizia zinahitajika shilingi 40,000,000/=.

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya utaratibu wa kutumia fedha za mfuko wa Tuzo na Tozo ili kumalizia ujenzi wa vituo mbalimbali vilivyosimama katika ujenzi kutokana na kukosa fedha kikiwemo Kituo cha Polisi Chukwani. Hata hivyo, kwa kushirikiana na wananchi na wadau werevu, Kituo hiki kitaendelea kukamilishwa ili kianze kazi ya kuwahudumia wananchi wa eneo hili na maeneo jirani. (Makofi)