Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 61 2021-04-13

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya kujaa maji mara tu mvua zinaponyesha katika baadhi ya maeneo ya Kata za Magomeni, Shangani, Ufukoni, Reli na Likombe katika Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto ya kujaa maji mvua zinaponyesha katika baadhi ya maeneo ya Kata za Magomeni, Shangani, Ufukoni, Reli na Likombe katika Manispaa ya Mtwara Mikindani. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali kupitia Mradi wa Uendelezaji Miji (Tanzania Strategic Cities Projects) imejenga mifereji ya kutoa maji kwa maana ya stand-alone drains yenye urefu wa kilomita 10 kwa gharama ya shilingi bilioni 1.82 katika Kata za Shangani, Reli, Likombe na Vigaeni Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kukamilisha Mpango Kabambe wa kuyaondoa maji ya mvua katika makazi na kuyaelekeza baharini katika Manispaa ya Mtwara Mikindani. Serikali itatafuta fedha ili kutekeleza kikamilifu Mpango Kabambe wa kuondoa maji ya mvua kwenye makazi na kuyaelekeza baharini katika Manispaa ya Mtwara Mikindani.