Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 60 2021-04-13

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuruhusu wananchi wanaoishi kwenye Miji ambayo ipo kando ya barabara kuu kama Mji wa Mafinga kufanya biashara kwa saa ishirini na nne?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kubuni mikakati mbalimbali katika kuwaendeleza wafanyabiashara wadogo ikiwa ni pamoja na kuwatengea maeneo kwa ajili ya kuendesha biashara zao na kuwatambua kwa kuwapatia vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo na watoa huduma. Kutokana na uhaba wa maeneo ya kufanyia biashara kwenye baadhi ya Miji, yameanzishwa masoko ya usiku ambayo yanaendeshwa kwa kufunga baadhi ya Mitaa nyakati za jioni hadi usiku kwa ajili ya kupisha wafanyabiashara wadogo kuendesha biashara zao. Baadhi ya Halmashauri hizo ni Jiji la Dodoma, Jiji la Dar-es-Salaam na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Mheshimiwa Spika, uendeshaji wa biashara nyakati za usiku umeonekana kuwa na changamoto nyingi za ulinzi na usalama wa wafanyabiashara, wateja pamoja na bidhaa zao. Uzoefu unaonesha kuwa maeneo zinakofanyika biashara kwa saa 24 kuna miundombinu yote muhimu ikiwemo taa, kamera, vyoo na maeneo ya kuhifadhia bidhaa za wafanyabiashara.

Aidha, ili kuwa na usalama wa uhakika katika masoko, kunahitajika ulinzi wa Polisi au Askari wa akiba kwa maana ya Mgambo, hususan nyakati za usiku. Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama itaendelea kutafuta namna bora ya kuwezesha wafanyabiashara waishio kwenye Miji kando ya barabara Kuu ikiwemo Mafinga kufanya biashara zao kwa saa 24 ikiwa ni pamoja na kuweka miundombinu ya msingi.