Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 16 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 132 2016-05-10

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:-
Katika Jimbo la Segerea kuna zahanati kumi lakini hakuna zahanati moja iliyopandishwa hadhi kuwa kituo kikubwa cha afya chenye uwezo wa kulaza wagonjwa.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuipandisha hadhi Zahanati ya Tabata „A‟ kuwa Kituo cha Afya kwa sababu ina miundombinu yote inayofaa kwa Kituo cha Afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali naomba nifanye correction ya data, kulikuwa kuna typing error hiyo mwaka 2015/2016 isomeke 2016/2017.
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, zahanati ya Tabata „A‟ haina eneo la kutosha kukidhi upanuzi wa miundombinu unaohitajika na hivyo inakosa sifa ya kupandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya. Ili zahanati iweze kupandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya inatakiwa kuwa na wodi ya wanaume na wanawake zenye vitanda 24 kila moja, jengo la upasuaji, jengo la wagonjwa wa nje (OPD), huduma za mama na mtoto, chumba cha kuhifadhia maiti na kichomea taka incinerator.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zahanati ya Segerea ina eneo la kutosha, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imetenga shilingi milioni 75. katika bajeti ya mwaka 2016/2017 ili kujenga wodi zinazotakiwa ikiwa ni maandalizi ya kuipandisha hadhi Kituo cha Afya. Taratibu za kupandisha hadhi zahanati kuwa Kituo cha Afya zinaanza katika Halmashauri yenyewe kupitia vikao vyake, hatimaye maombi hayo yatawasilishwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ili kuipatia kibali.